A joint initiative by the United Nations, The Government of Tanzania and The Economic and Social Research Foundation  

A platform for professionals and experts to meet, share and exchange experiences
Username >

Password >

Forgot | Change Password? Register! Home
Topic : Nini Kifanyike Baada ya Muda wa Malengo ya Milenia – 2015 Ili Kuongeza Kasi na Kutoa Msukumo Wa Maendeleo katika nchi yetu?  
 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania,kupitia Ofisi ya Raisi- Tume ya mipango imeanzisha majadiliano ya Wadau kitaifa yanayohusu mchakato wa Maendeleo baada ya kufikia kipindi cha Malengo ya Milenia, mwaka 2015.

Itakumbukwa kuwa Tanzania ni moja ya mataifa 189 ambayo mnamo mwezi Septemba m ...Click here to read more

     
Comments From TAKNET Members
Zaynab Makongo Iddy  : Saturday, March 2, 2013    
  Mie ninachoona kifanyike kwanza kabla ya yote ni kupata viongoz walio waadilifu na wenye uzalendo wa taifa lao...  
     

ojung loy  : Friday, December 14, 2012    
  Millenium goals yamefikiwa kwa kiwango kidogo ktk nyanja zote,hii imetokana na either viongoz kutokuwa na uzalendo,uchungu na hata commitment ktk kusimamia rasilimali ambazo kama proper utilisation ingefanyika ktk misingi ya haki na usawa tungevuka malengo may be dhana ya hatuwezi ingekufa kwa wenye dhamana kuwa na spirit ktk kuleta mapinduzi kwa vitendo kuliko maneno ktk media,lets us leave difference ideology of political issues to build our nation  
     

Donald Dickson Kibhuti  : Monday, December 10, 2012    
  Ni kweli, malengo ya milenia yamefikiwa kwa kiwango ambacho si malengo yaliyotarajiwa.

Hali hii imesababishwa na mambo yafuatayo:

Kwa upande wa mazingira, hasa mali asili imeendelea kutoweka bila kuleta matarajio tuliyotegemea hasa kupunguza umaskini wa watanzania. Sasa bado hali ya uchumi kwa mtu mmoja mmoja ni mbaya na mwananchi huyu anaishi maisha duni, ingawa uchumi wa nchi unaongozeka lakini haujasaidia wananchi wa kawaida ambao bado wapo kwenye lindi la umaskini.

Hii hali inatisha, hizi raslimali zinakwisha lakini bado hazijaleta unafuu wa kimaisha.

Pili, elimu haijahimizwa kama mkazo kwa ajili ya kuwakomboa vijana kifikra. Hivyo vijana bado wana umaskini wa kifikra, hapa ndipo panatakiwa mkazo na serikali kuwatoa wananchi wake katika umaskini wa kifikra na iamue kuwekeza rasilimali zake nyingi ili vijana na rika zote waweze kujitambua na kuwa matajiri wa fikra ili waweze kuzitumia fursa zilizopo ili kuwatoa katika umaskini huu mbaya kuliko umaskini mwingine.

Huduma za afya bado haziridhishi. Huduma hizi zimeelekezwa mijini na kuwasahau watu wa vijijini hasa wanawake na watoto wamekuwa waathilika wa huduma duni zinazotolewa na serikali na kusababisha vifo vya wamama wajawazito na watoto kuendelea kuongezeka.

Kuhusu siasa, hili ni janga linaloitesa jamii ya watanzania kwani wao wamekuwa ni daraja la kuwapeleka watanzania katika lindi la Umaskini, kwa sababu wanasiasa ndio watawala wa rasilimali walizokabidhiwa kuzilinda kwa maslahi ya watanzania lakini badala ya kuzilinda, wamezitumia kujinufaisha binafsi na familia zao badala ya kuwanufaisha watanzania walio wengi. Huu ubinafsi unaowanufaisha tabaka la watawala, umeeleta umaskini kwa watanzania wengi. Mfano, mtawala anapokea rushwa ya pesa ili auze rasilimali kwa bei ya kutupwa. Hili inakuwa imemnufaisha mtawala na familia yake na wala sio watanzania. Hapa Mungu tunamuomba arudishe upendo wa watawala kwa watanzania

Serikali inatakiwa kufanyia kazi maeneo yote niliyoainisha ambayo ni machache.

Mungu ibariki Tanzania

 
     

Nellie John Mwandoloma  : Monday, December 10, 2012    
  "Makundi ya watoto wanaoshi katika mazingira hatarishi hususani wa mitaani" Nionavyo, ni kuwa jambo hili linashughulikiwa na watu wengi, kwa bahati mbaya si wote wenye dhamira ya dhati katika kushughulikia watoto hawa.Napendekeza serikali ichukue jukumu la kuliangalia jambo hili kwa uzito wake.Asasi mbalimbali zipewe nafasi ya pili, badala ya ilivyo sasa kuwa asasi zinachukua nafasi ya kwanza! Kwa pamoja Watanzania twaweza kulitatua tatizo hili, kwa kutumia rasilimali tulizonazo kuanzia ngazi za wilaya.  
     

Novatus  : Friday, December 7, 2012    
  a) Makundi ya watoto wanaoshi katika mazingira hatarishi hususani wa mitaani

b) Ni kitu gani kimeyafanya maisha kuwa mabaya siku za karibuni(umaskini,kuzaa bila mipango na utaratibu kamili,migongano katika ndoa na familia,halmashauri za wilaya kutokuwa na mipango madhubuti na rasilimali za kutosha kushughulikia makundi hayo na kuona kuwa hili ni tatizo la kushughulikiwa na wahisani.

Nini kifanyike kurekebisha hali ya kutoishi maisha mazuri? watoto waliopo mitaani waondolewe;halimashauri za wilaya ziangalie upya masuala ya kiustawi kwa kuweka mikakati inayolenga kuboresha uchumi na ustawi wa kaya na mtu mmoja mmoja,miongozo na hata sheria ndogondogo pia kuimarisha na kuboresha idara ya ustawi wa jamii

c) Kitu gani kifanyike na lini kifanyike ili kuwezesha watu kuishi maisha bora? sawa na hapo juu na hiyo ianze utekelezaji sasa

d) Ni nini kinahitajika ili kufanikisha hayo mapendekezo? uchambuzi wa kina wa tatizo, utayari wa serikali kuondoa tatizo hilo,rasilimali watu(wenye nia,ujuzi na maarifa ya kutosha),fedha na vifaa.

 
     

Abdallah Hassan  : Thursday, December 6, 2012    
  Ndugu

Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania,kupitia Ofisi ya Raisi- Tume ya mipango imeanzisha majadiliano ya Wadau kitaifa yanayohusu mchakato wa Maendeleo baada ya kufikia kipindi cha Malengo ya Milenia, mwaka 2015. Malengo ya Milenia ni makubaliano yanayozitaka nchi zote zilizoendelea na zinazoendelea kufanya kazi kwa pamoja kufanikisha malengo hayo.

Kwa kifupi Malengo ya Milenia yanayoishia mwaka 2015 yanasisitiza maendeleo katika maeneo ya afya, elimu, mazingira na ustawi wa jamii kwa ujumla.

Tanzania ni kati ya nchi zilizoitikia wito wa Malengo ya Milenia, na imefanya vizuri katika maeneo mengi, ingawaje matokeo katika baadhi ya maeneo sio ya kuridhisha.

Kwa kuwa sasa hivi tunakaribia kufikia mwisho wa Malengo ya Milenia, na kwa kuwa baadhi ya nchi bado hazielekei kuyafikia Malengo ya Milenia ifikapo 2015 kama tulivyotegemea. TAKNET inaungana na tasisi zingine kukusanya maoni yenu ili kupata vipau mbele kitaifa ili kupanga mikakati endelevu ambayo wewe miongoni mwa wadau unaamini kuwa itakuwa na ufanisi. Taarifa itakayotokana na majadiliano haya, itachangia katika kuandaa mikakati mipya na malengo mapya tunayoamini yatatoa msukumo wa kimaendeleo duniani kote, hususani katika nchi yetu.

Mjadala huu uzingatie pamoja na mambo mengine maswali yafuatayo:

a) Makundi yepi ya watu hawaishi maisha mazuri katika jamii utokayo?

b) Ni kitu gani kimeyafanya maisha ya watu kuwa mazuri au kuwa mabaya siku za karibuni, na nini unadhani kifanyike kurekebisha hali ya kutoishi maisha mazuri?

c) Kitu gani kifanyike na lini kifanyike ili kuwezesha watu kuishi maisha bora?

d) Ni nini kinahitajika ili kufanikisha hayo mapendekezo?

Mjadala huu unasimamiwa na:

Dr. Oswald Mashindano

Dr. Tausi Kida

Mrs. Margareth Nzuki

Mrs. Vivian Kazi

Mr. Abdallah Hassan

 
     

  This topic has been closed. You can only view comments!  
     

 

 

  ESRF
  Tanzania Development Gateway
  Tanzania Online
  Government of Tanzania
  United Nations (UN)
More»
 
v  
v TOP CONTRIBUTORS
  Omari Mwinyi Khamis(156)
  Festo E. Maro(69)
  Abdallah Hassan(49)
  japjet Makongo(30)
  Kabuje Furaha(26)
   
All Contributors»



 
Tanzania Knowledge Network (TAKNET) Platform is supported by The Government of United Republic of Tanzania,
United Nations Development Programme (UNDP) and coordinated by Economic and Social Research Foundation (ESRF).


Disclaimer | About Us | Feedback | Membership | Contact Us | Admin
© 2015 Economic and Social Research Foundation. All Rights Reserved.